Tuesday, May 20, 2008

Lipo tatizo la msingi ambalo sisi kama Watanzania au Waafrika tumegoma kabisa kulipa mjadala wa kina. Tunaogopa kabisa kuligusa kwa sababu ambazo kimsingi nilikwishazijadili huko nyuma.

Tatizo ni kwamba nchi hii haina misingi ya kile inachokiamini kwa dhati ambacho watu wake wanaweza kukipigania hata kama watakufa wakiwa wanakipigania. Msingi mkuu sasa hivi ni pesa. Kila mtu anapigania tumbo lake na la watoto wake.

Na kutokana na mlolongo wa matukio, na pia ukweli nilioueleza hapo juu ninaweza kabisa kuvaa joho la Sheikh Yahya Hussein na kutabiri kwa hakika kwamba kabla mwaka huu au kipindi hiki cha kwanza cha Rais Kikwete hakijafika ukingoni basi kutakuwa kumetokea mabadiliko zaidi katika Serikali.

Bonyeza hapa

No comments: