Friday, February 29, 2008

TBS INATUKWAZA

Hakuna kitu kinachovutia kama unapoenda dukani kununua kitu ukakuta kitu hicho ndio kile kile unachotaka wewe na ubora ni ule ule ulioutegemea kutokana na matangazo uliyoyaona yanayohusu bidhaa hiyo .

Pia hakuna kitu kinacholeta huzuni unapoenda dukani kununua kitu ukaambiwa ni bora kabisa , na ndicho hicho unachotaka na ulitegemea kutokana na tangazo hilo hilo .

Lakini kitu hicho kina baadhi vya vifaa vimebadilishwa au kuwekewe vingine ambavyo havina ubora unaotakiwa na havikidhi matajio yako na masoko yako .

Wewe hujui kwa sababu ni mtumiaji tu huwezi kukagua ndani kujua vitu vingine zaidi au labda wakati unaenda hukupata ushauri kutoka kwa wataalamu wakuambie hili na lile wewe umeenda tu .

Na ndio hivyo umeshanunua kitu hicho umetumia miezi 2 kitu kimekufa data zako kule ndani zimepotea , ukifungua ndani katika hicho kifaa kuna maandishi pale HATUHUSIKI NA UPOTEVU WA DATA ZAKO umeshauwawa tena .

Ukienda dukani unaambiwa kifaa chako kimepata matatizo ya umeme kwahiyo hatulipi vitu vinavyokufa kwa sababu za umeme , unachotakiwa ni kununua vingine .

Haya sasa umeamua kuonana na wataalamu wanaiangalia , wale wanaojua zaidi wataenda katika mtandao kuangalia serial number ya hicho kifaa chako kama kweli kimetengenezwa na kampuni husika .

Unagundua kwamba HP COMPAQ hawana bidhaa yenye serial number zilizoko katika computer hiyo , ukiangalia model hiyo huwa inakuja na HDD za aina gani , unakuta HP COMPAQ original huwa zinakuja na HDD za aina Fulani ambazo katika ile yako sio ile .

Sasa utaenda kulalamika wapi ? ukienda TBS hakuna wa kukusikiliza au unatakiwa uandike maelezo marefu sana , huwezi kwenda kushitaki wakati mwingine kwa sababu hawa wadosi si unawajua wewe mwenyewe ndio unaweza kuumbuka .

TBS inatakiwa iwe macho sana na hizi bidhaa bandia zinazoingizwa nchini bila kufuatilia maadili ya bidhaa hizi na hata mashirika ya umma yanaponunua bidhaa hizi basi wahakikishe taasisi za kudhibiti ubora wanaangalia nakujua ubora au na kama zinakidhi mahitaji ya sehemu husika .
TBS iweke mambo yake wazi jinsi inavyoshugulikia mambo haya yanayohusu vifaa hivi , watoe namba zao wazi , emails na kadhalika iwe rahisi watu kuwasiliana nao zinapotokea shida kama hizi .

Unaona kama hapo juu umenunua bidhaa ya hp ambayo ni bandia hakuna wa kumlalamikia zaidi ya hp wenyewe , na wenyewe watasema hatuyatambui maduka hayo yanayouza hizo bidhaa na hatuna mkataba nao wowote ule .

Monday, February 25, 2008

















Wednesday, February 20, 2008


Kuna usemi usemao "mafanikio ya mwanaume kwa kiwango kikubwa(100%) huchangiwa na mwanamke" kwa maelezo zaidi tembelea tovuti http://damija.blogspot.com/

Tuesday, February 19, 2008




Waliopigwa Kiteto....

Huyo ni kiongozi wa Chadema Bw. Baraka Daudi baada ya kupewa mkong'oto kwenye Kituo cha Polisi huko Kiteto.




Hawa ni viongozi wengine wa Chadema wakiwa kituo cha Polisi baada ya kupigwa wakiwa mikononi mwa Polisi.







Monday, February 18, 2008

Karibu Raisi Bush















Raisi George Bush wa Marekani akiwa ameongozana na mkewe wamewasili katika Kiwanja cha Ndege jijini Dar es Salaam

"Sema mwanahabari “
“ Shetani anakuja saa ngapi ?”
“ unaonaje msimamo wa waisilamu ?”

Huyo ni rafiki yangu mmoja alinipigia simu jana usiku katika maongezi yetu kwanza alianza kwa maneno na maswali hayo hapo juu , mimi nilibaki nimeduwaa tu kwanini anamwita bush shetani .

Sikutilia maanani sana anavyomuita bush shetani , kwa sababu hilo neno sasa limeshakuwa la kawaida na ni propaganda tu kama zingine , nilishituka alivyoniuliza kuhusu msimamo wa waisilamu katika suala zima la ujio wa bush .

Nilimwambia maneno machache kwanza atambue Tanzania ni nchi ambayo haina dini , ni nchi huru na watu wake wako huru , mtu anaweza kusema na kuongea chochote bila kuzuiwa ili mradi asivunje sheria za sehemu husika kila sehemu inasheria zake kutegemea na eneo alipo msikitini , kanisani , jamatini kila sehemu na lake .

Kwa kuwa watu wake wako huru , hata waisilamu nao wako huru kusema kile wanachotaka , kama wamekifanyia utafiti na kuwa na uhakika nacho na kwa uhakika walifanya maandamano jana kuelezea hisia zako kuhusu sera za taifa hilo za kimataifa .

Inawezekana hata leo wakaandamana tena kwa sababu hatujui jana walikubaliana nini baada ya maandamano yao , kwahiyo tusiwapuuze tu na kuacha mambo haya yafe hivi hivi .

Kama taifa lazima lifikirie kilio cha hawa waisilamu wachache kwa sababu ni sehemu ya Tanzania , kizazi hichi kitakuwa na fikira hizo na chuki hizo dhidi ya taifa la marekani kwa miaka mingi ijayo , mfano niliona moja ya malalamiko yao ni kuhusu baadhi ya masheikh kukamatwa na miradi yao kufungwa

Je nani anapenda miradi kama ya zahanati , shule na maendeleo mengine zifungwe kwa sababu ambazo haziko wazi kama hawa waisilamu wanavyojaribu kusema ? wao wanahusisha hayo na bush .

Pamoja na yote haya waisilamu wasimlaumu bush na serikali yake kwanza wajiulize kuhusu hawa masheikh wao waliokamatwa kama wanavyosema na miradi yao iliyofungwa , waweke mbali hisia zao za kidini watuambie hawa mashekh ni kina nani na ni mali ghani za waisilamu zilizofungwa au kusimamishwa .

Wasipokuwa wazi basi tutaendelea kuamini kwamba tatizo sio bush tatizo ni la waisilamu wenyewe na mambo yao , haswa hivi vikundi vichache , na hivi ndio vikundi ambavyo vilituletea balaa uwanja wa taifa katika sakata la kwenda mecca .

Hivi vikundi lazima tuwe navyo makini sana , na tuviangalie kwa karibu wasiposikilizwa wanaweza kuanza kulipa visasi kama tunavyoona katika nchi zingine haswa mashariki ya kati

Thursday, February 14, 2008


“Kumbadili waziri, hata Waziri Mkuu, si jambo la ajabu. Anaweza kujiuzulu, anaweza kufukuzwa, na nchi isitikisike. Lakini huwezi kumtikisa Rais wa nchi bila kuitikisa nchi yenyewe. Ni vizuri jambo hili likatamkwa waziwazi na likaeleweka sawa sawa. Maana watu wengine wananong’ona nong’ona kuwajibika kwa Rais kana kwamba ni jambo la mchezo mchezo tu.
Kulazimika kumchukulia hatua Rais wa nchi ni mkasa na balaa kwa nchi yoyote ile. Ndiyo maana tunatakiwa kuwateua na kuwachagua marais wetu kwa uangalifu mkubwa, na ndiyo maana wakisha kuchaguliwa, wanatakiwa kujiheshimu na kuwa waangalifu sana.” - Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
LAZIMA nikiri kuwa niliyakumbuka maneno haya mara tu baada ya Edward Ngoyai Lowassa, kutangaza kuwa alikuwa amewasilisha barua kwa Rais Jakaya Kikwete, ya kutaka kujiuzulu wadhifa wake wa Waziri Mkuu, kutokana na kuhusishwa na kashfa ya Richmond.
Maneno hayo yamo katika kitabu cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kiitwacho “Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania.” Mwalimu alikiandika kitabu hiki, nusu ya mwanzo ya miaka ya ‘90, baada ya nchi kutikiswa na mambo matatu makubwa: Mosi, ilikuwa ni hatua ya Zanzibar kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC). Pili ilikuwa ni utaratibu mpya wa kumpata Makamu wa Rais, yaani chini ya mfumo wa vyama vingi. Na tatu ni wabunge wa Tanzania Bara walipodai serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano.
Kwa hiyo, inatosha kusema tu kwamba, kwa kiasi kikubwa, niliposikia uamuzi wa Lowassa, nilikikumbuka kitabu hicho. Sitazungumzia suala la Richmond katika makala hii. Lakini ninataka kuwasilisha mtazamo wa Mwalimu Nyerere kuhusu suala la wakubwa kujiuzulu kwa hiari pale wanapokoroga mambo au mambo yanapoelekea kuwakoroga.
Nilipoangalia kwa makini Mwalimu anajikita zaidi kwa nafasi za mawaziri na Waziri Mkuu, ambao wanapaswa kuachia ngazi pale mambo yanapovurugika chini ya usimamizi wao.
Watu wengi wamesikika wakisema kwamba tamko la Lowassa la kujiuzulu uwaziri mkuu, lilikuwa limeitikisa nchi. Inawezekana. Lakini kwa mtazamo wa Mwalimu Nyerere, “kumbadili waziri, hata Waziri Mkuu, si jambo la ajabu. Anaweza kujiuzulu, anaweza kufukuzwa, na nchi isitikisike. Lakini huwezi kumtikisa Rais wa nchi bila kuitikisa nchi yenyewe.” Kwa mtazamo huo wa Mwalimu, nchi inaweza tu kutikisika endapo tu Rais ataguswa.
Mara nyingi suala la kujiuzulu kwa mawaziri au hata Waziri Mkuu, limekuwa ni suala la vuta nikuvute. Waziri anaweza kuhusishwa na kashfa fulani, lakini zinapokuja hoja za kutaka ajiuzulu, anakuwa kama hasikii kitu.
Pengine mfano pekee katika historia ya nchi hii, (ukiondoa huu wa Lowassa), ni ule uliomhusu rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi. Akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, watumishi walioko chini ya wizara yake, huko Shinyanga, walisababisha vifo vya mahabusu. Ilibidi aachie ngazi kwa hiari yake, na hatua hiyo ilimjengea heshima.
Katika kitabu chake, “Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania”, Mwalimu Nyerere anasema: “Pengine inafaa niseme kwamba inashangaza na kutisha kidogo, kuona kuwa kujiuzulu kwa waziri yeyote kunafanywa kuwa ni jambo la kuvutana au la kubembelezana.
“Ndugu Ali Hassan Mwinyi aliwahi kuwaa Waziri wa Mambo ya Ndani katika Serikali ya Muungano. Makosa fulani yalifanyika katika wizara yake. Hakuwa amefanya yeye, yalikuwa yamefanywa na watendaji fulani walio chini ya wizara yake. Alilazimika kubeba lawama, akajiuzulu. Nadhani kuna wengine waliolazimika kujiuzulu kutokana na mkasa huo huo.”
Huo ndio msimamo wa Mwalimu kuhusu dhana ya uwajibikaji, hata kama mhusika hakushiriki kutenda kosa, ili mradi tu dosari imefanyika chini ya dhamana yake.
Lakini pia Mwalimu anazungumzia suala la kumbadilisha Waziri Mkuu, kuwa si kitendo cha ajabu. Na hapa anarejea mfano wa jinsi alivyomwondoa Waziri Mkuu, Rashidi Kawawa na kumwingiza Edward Moringe Sokoine. Mwalimu anazungumzia tukio hilo kwa maneno yafuatayo:
“Wala kubadili Waziri Mkuu si jambo la ajabu. Ndugu Rashidi Mfaume Kawawa alikuwa ni Waziri Mkuu wangu kwa muda mrefu. Hakuwa amefanya kosa lolote; lakini nilitaka kumbadili na kuteua Waziri Mkuu mwingine. Nilimwita, nikamwambia hivyo. Tukakaa pamoja mimi na yeye, tukashauriana na kukubaliana ni nani anafaa kushika nafasi yake. Nikamteua Edward Moringe Sokoine. Najua kuwa watu wa aina ya Rashidi Kawawa ni adimu sana duniani, hawazaliwi kila siku.
“Ni jambo la kushangaza kidogo kwamba viongozi…wanaona kuwa ni kosa kuwakumbusha kuwa vyeo walivyo navyo ni dhamana. Wanadhani kuwa uwaziri ni usultani: ukishakuwa sultani utakufa ukiwa sultani! Nadhani wanakosea. Nchi hii imewahi kung’oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wa kuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa.”
Hata hivyo, pamoja na mtazamo wake kuhusu kujiuzulu, Mwalimu Nyerere anarudi nyuma kuhusu ugumu wa kudhibiti makosa yasitendeke katika mchakato mzima wa utendaji kazi. Kwamba huwezi kujijengea utaratibu wa kuzuia kabisa makosa yasifanyike. Lakini anasema kwamba yakifanyika hakuna budi wahusika wawajibike. Namnukuu:
“Hatuwezi kujijengea utaratibu wowote ambao utazuia kabisa makosa yasifanyike, hata makosa makubwa. Lakini tunatazamia kuwa yakifanyika, wanaohusika watawajibika.
“Na katika makosa makubwa ya maadili na utendaji, mwenye jukumu la wazi wazi la kuwadhibiti wahusika ni Rais. Mawaziri wake wanapofanya makosa makubwa, na badala ya kujiuzulu waanze kufanya hila na kutafuta visingizio vya kutofanya hivyo, ni wajibu wa Rais kuwafukuza, na tunamtazamia kufanya hivyo.
“Ni kazi yake mwenyewe, asiyoweza kusaidiwa na mtu mwingine. Mtu anaweza kumsaidia Rais kumnong’oneza waziri wake kujiuzulu, lakini hawezi kumsaidia kufukuza waziri wake. Hiyo ni kazi ya Rais peke yake. Asipoifanya, kosa ni lake peke yake.”
Kwa mantiki hiyo, mawaziri waliojiuzulu sambamba na Waziri Mkuu, Edward Lowassa, yaani aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Ibrahim Msabaha, wangeweza kuondolewa tu na Rais pekee endapo wasingetamka kuachia ngazi zao kwa hiari.
Na kama mawaziri hao wawili wangebaki kimya na Rais naye akanyamaza, basi hakuna mwingine zaidi ambaye anaweza kuingilia kati, isipokuwa tu manung’uniko na minong’ono ya hapa na pale mitaani.
Pengine jambo la msingi ambalo limeleta mabadiliko makubwa ya uongozi wa Awamu ya Nne wiki iliyopita ni pale wachache walipopiga moyo konde na kuuweka pembeni woga. Na hapa naweza kurejea wajumbe wa Kamati ya Bunge, iliyochunguza kashfa ya Richmond.
Nasema waliweka woga pembeni kwa kuwa mmoja wa viongozi waliyekuwa wakimgusa katika uchunguzi wao alikuwa ni Waziri Mkuu. Hapa palihitaji kupiga moyo konde kweli kweli.
Lakini pia kulikuwa na ujasiri upande wa wabunge. Ujasiri wao huo ulianza pale walipoikataa semina ya Wizara ya Nishati na Madini, ambayo ilikuwa iegemee kwenye suala la Richmond.
Nasema huu ni ujasiri kwa kuwa kumekuwa kukisika kauli za mara kwa mara, kwamba Bunge letu ni rubber stamp, yaani ni mhuri tu wa kupitisha matakwa ya Serikali. Bahati nzuri wabunge wameapa kuwa kitu kimoja katika masuala yanayohusu maslahi ya taifa.
Mwalimu katika kitabu chake anakemea suala la woga. Anasema: “Kukubali kufanywa vikaragosi vya viongozi ni dalili ya woga. Si dalili ya heshima. Na woga na heshima ni vitu viwili mbali mbali. Maadili mema yanatutaka tuheshimu viongozi wetu, madhali wanajitahidi kutimiza wajibu wao.
“Maadili mema hayatudai tuwaogope viongozi wetu. Na viongozi makini hupenda kupata heshima ya wananchi wenzao, lakini hawapendi kuongopwa. Kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta. Viongozi halisi hawapendi kushiriki. Kujenga mazoea ya kutii viongozi, hata katika mambo haramu ni dalili ya woga, ni kukaribisha udikteta.”
Edward Lowassa kaachia uwaziri mkuu. Nazir Karamagi kaachia uwaziri wa Nishati na Madini na Dk Ibrahim Msabaha kaachia nafasi kama hiyo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwa kiasi fulani, nadhani, Mwalimu anaweza kuwa anageukageuka kwa furaha kaburini kwake kutokana na uamuzi wao na matarajio yake.


kwa kweli huyu Mheshimiwa Harrison Mwakyemebe na kamati yake ninawaheshimu sana kwa jinsi walivyofanya kazi hii.

Je, Mnakumbuka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!akiapa kuilinda Katiba alipoapishwa kuwa Waziri Mkuu

Pichani Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa (CCM)
Hatimaye mchawi wa Richmond ni yule ambaye watu walimhisi kwa muda mrefu. Na sasa tumegundua hakuwa peke yake. Taarifa ya leo ya Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa mwishoni mwa mwaka jana kuchunguza mkataba wa Richmond imeonesha kuwa siyo tu taratibu zilikiukwa bali pia kuna ushahidi mkubwa wa rushwa


Ripoti hiyo ambayo inaonesha wazi kuwa mhusika mkubwa wa sakata hili zima ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa vile bwana Lowassa aliapa kuilinda na kuitetea Katiba yetu na kwa vitendo vyake ameshindwa kufanya hivyo hana budi kuwa wa kwanza kuwajibika yeye mwenyewe bila ya kungojea kuwajibishwa. Mhe. Lowassa kwa hili umekosea na liwe somo kwa viongozi wengine wote kuwa Tanzania inabadilika na viongozi wasioongoza hawana budi kuwekwa pembeni. Mhe. Lowassa tunataka ujiuzulu wadhifa wako mara moja


Pamoja na wewe wahusika wengine wote ambao wanatajwa katika ripoti hiyo akiwemo Waziri Msabaha, Karamagi, Rostam Aziz na Mwanyika nao pia wajiuzulu mara moja kwa kutumia madaraka yao vibaya, kulidanganya Taifa, kufanya kazi kinyume na maadili, na kwa kuliletea Taifa letu hasara.


Watanzania wana mambo mengine ya msingi ya kufuatilia (kama BoT na mengine) na wakati umefika suala la Richmond lifikie kikomo kwa viongozi na wahusika wote kujiuzulu. Tulishasema toka awali kuwa Baraza hili la mawaziri ni la kishikaji na ambalo limemwangusha sana Rais na kwa hakika ni kujiangusha alikojitakia kwani alishaonywa, halina budi kuvunjwa ili Baraza jipya litakalokidhi hamu na matamanio ya Watanzania na ambalo wajumbe wake watatoka hata nje ya CCM liundwe ili tuendelee na jitihada za kulijenga Taifa letu


14/2/....... nisiku maarum kwa watu wapendanao (familia, Marafiki) nisiku ambayo hasa hasa husherekewa na Vijana lika kati ya 14-25 ndio huwa na moto sana. Valentine sio ngono ila watu wanaipeleka kuwa ngono kwa kufanya mambo yasiyostahili kitu kina jenga hisia mbaya kwa jamii. Nawashauri siku ya leo 14/2/2008 jitahidi kuangaria wapi hukuwa sawa ktk mahusiano either ya Mume& Mke (Familia kwa ujumla + watoto), Jamii inayokuzunguka, na Marafiki jirudi na uanze upya niwakati wa kupanga na wenzi wako.


Catherine & Shumbusho wanawatakia watanzania wote Heri ya Wapendanao


JK akiteta jambo na Waziri Mkuu Mpya pamoja na Makamu wake.

Unaweza kuwemo!

Baraza jipya la mawazili


Rahisi wa Jamuhuli ya Muungano wa Tanzania akiwa na makamu wa rais d. ali mohamed shein na waziri mkuu mh. mizengo pinda pamoja na baraza jipya la mawaziri baada ya kuliapisha leo ikulu ndogo ya chamwino, dodoma

Tuesday, February 12, 2008

BUNGE LA TUKUFU LA TANZANIA:

MWENYEKITI TUME TEULE YA BUNGE: "Waziri Mkuu ameshiriki katika kuibeba Richmond" pwa pwa pwa pwaaaaaaaaaaaaaaa MAKOFIIIII (JANA

WAZIRI MKUU : "Nimemwandikia Rais barua ya kubwaga manyanga. Lakini sikubaliani kabisa na taarifa ya Kamati Teule ya Bunge. Ni mambo ya siasa za Dar Dar es Salaam. Kwanini wasinihoji. Wamenionea.. ..." Pwa pwa pwa pwaaaaaaaaaaaaaaa MAKOFIIIII (LEO)

BUNGE LETU HILO, BWANA

WACHA NA TUSIKIE MJADALA JIONI NDANI YA JUMBA. NA TUSIKIE RAIS ANASEMAJE. LAKINI YOTE KWA YOTE,KAMATI IMETIMIZA WAJIBU WAKE BARA BARA. NA WAZIRI MKUU KACHUKUA HATUA MUAFAKA (Hata kama kwa kuchelewa maana kelele zilishakuwa nyingi juu ya Waziri Mkuu. BADO LA MVUA YA 'WAGANGA WA THAILAND???? )

Nawasilisha

Hizi ndizo amri kumi za Tanzania, kama unataka kuinusuru Tanzania isiuzwe inakubidi izufuate:-
1. Usiwe mlaghai kama Karamagi

2. Usiwe fisadi kama Balali

3. Usiwe mbishi kama Zitto

4. Usiwe makelele kama Makamba

5. Usiwe mbabe kama Sitta

6. Usihukumu kama Mudhihiri

7. Usiuwe kama Ditopile

8. Usidandie hoja kama Mrema

9. Onea huruma nchi kama Dr. Slaa

10. Usiwe na tamaa kama Lowasa

Tanzania ya Nyerere: Mafunzo ya maendeleo, umoja na amani

Mgomo wa 6 wa Wanawake Duniani – Machi 8 2005
Wapendwa ndugu zangu,
Komesha Umasikini na Vita – Wekesha katika Kutunza na siyo Mauaji!
Malipo kwa kazi zetu na sawazisha malipo kwenye soko la Dunia
Kila iliposherehekewa Siku ya Kimataifa tangu Mwaka 2000,Wanawake katika zaidi ya Mataifa 60 wametumia kila hatua za pamoja kuanzia ngazi ya chini wakiitaka jamii iwekeze katika kutunza badala ya mauwaji, na kwamba fedha zinazoharibiwa kugharimia vita zingetumiwa badala yake kutimiliza mahitaji ya jamii. Mgomo huu umezidi kua imara katika kipindi cha miaka mitano,hususan katika Mataifa ya kusini mwa Dunia, ambapo wanawake na pia idadi ya wanaume inayozidi kuongezeka, kwa pamoja wanazingatia hatua hizi kila kukicha. Tumejionea jinsi manufaa ya ushirikiano wa kimatifa bila kujali mipaka .

Kupinga vita na kukomesha umasikini ni masuala mawili yasiyotengeka. Janga la hivi karibuni la Tsunami liliua karibu ya watu 300,000, lakini kila siku watu wanauawa kwa njaa,magonjwa, joto linalosababishwa na uharibifu wa mazingira pamoja na vita-yote yanayosababishwa na utawala wa uroho wa pesa na soko. Serikali pamoja na wapenzi wao wadhamini wa Kimataifa wanazungumzia bila kutimiza jinsi ya kukomesha umasikini lakini hawajawahi kutaja uwezekano wa kutukabidhi fedha tunazohitaji. Ni sisi wenyewe, tukianza na wanawake walezi wanaohangaika kila kukicha kuhifadhi maisha, juhudi zisizo lipiwa, ndiyo tutaweza kutekeleza mabadiliko haya. Mgomo ndiyo mfumo wetu wa kujiandalia lengo hili.
Madai ya Mgomo
· Malipo kwa kazi zote za huduma –katika mishahara,pensheni ya uzeeni,ardhi na njia nyingine za mapato.Nini la thamani kuliko malezi ya watoto na kuwatunza wengine? Wekeza katika uhai na mahitaji ya kimaisha,siyo bajeti ya majeshi au magereza.
· Usawa wa malipo kwa wote,wanawake kwa waume katika soko la Kimataifa.
· Upatikanaji wa chakula kwa mama anayenyonyesha, malipo ya likizo ya uzazi na likizo ya kujifungua. Komesheni kutuadhibu kwa sababu ya kuwa wanawake.
· Msilipe madeni ya Dunia ya Tatu’ Hatudaiwi ila tunawadai wao.
· Upatikanaji wa maji safi,huduma za afya,malazi, usafiri na elimu.
· Nguvu na Teknolojia zisizo haribu mazingira ambazo hufupisha saa za kazi.Wote tunahitaji majiko ya kisasa,majokofu, mashine za kufulia,kompyuta na mda wa kupumzika!
· Ulinzi a hifadhi dhidi ya fujo na unyanyasaji, pamoja na unaofanywa na watu katika familia na viongozi walio madarakani.
· Uhuru wa kusafiri. Hela inaruhusiwa kusafirishwa bila pingamizi,kwanini watu wasiwe na uhuru kama huo?

MAONI YA WANAHARAKATI KUHUSU RIPOTI YA RICHMOND ILIYOWASILISHWA BUNGENI DODOMA 06/02/08

MAONI YA WANAHARAKATI KUHUSU RIPOTI YA RICHMOND ILIYOWASILISHWA BUNGENI DODOMA 06/02/08

Wanaharakati wa masuala ya Jinsia, Haki za Binadamu na ukombozi wa wanawake kwa pamoja tunawapongeza wabunge wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania hususan walioanzisha hii hoja nzito na kuibua mjadala mzito wa Kitaifa, Kamati Teule, Vyama vya siasa, vyombo vya habari na wanaharakati wote kwa kuonyesha uzalendo juu ya mali za Taifa la Tanzania kwa kuweza kufichua na kuweka wazi mkataba wenye utata wa Richmond.

Pia tunawapongeza kwa kuona dalili kuwa Bunge limeanza kurudisha hadhi yake na tunatambua kuomba radhikulikofanywa na Spika wa Bunge kutokana na kauli yake kutumia neno ‘kukurupuka’ dhidi ya Naibu Spika wa Bunge
Tunalitaka Bunge lisirudi nyuma bali liendelee kusonga mbele kutetea na kusimamia maslahi ya wananchi

Sisi wanaharakati tunadai yafuatayo:
· Ripoti ya Kamati Teule ya Mkataba wa Richmond ichukuliwe kwa uzito wake kama ilivyo na iheshimiwe.
· Wahusika wote waliotajwa ( iwe Taasisi au mtu mmoja mmoja ) wawajibishwe kulingana na misingi ya Katiba na Sheria.
· Liundwe baraza jipya la mawaziri kufuata maadili ya uongozi
· Mikataba mipya inayotarajiwa kusainiwa iwe wazi na shirikishi
· Kamati ya Rais ya madini na ya BoT zibadilishwe na kuundwa kwa Kamati za Bunge za kuchunguza masuala ya madini, BoT pamoja na masuala yote ya raslimali za Taifa hili hususan katika vipindi vya urekebishaji wa uchumi.
· Mikataba yote yenye utata ifuatiliwe upya na iwe wazi
· Taasisi ya kudhibiti na kuzuia rushwa (TAKUKURU) iwe chini ya Bunge la Jamhuri ya Tanzania
· Mali yote ya Taifa iliyopotea irejeshwe
· Turejee ripoti ya Warioba ya mwaka 1996 kama kweli tunahitaji kupingana na ufisadi wowote ule
· Tunatoa angalizo kwa Spika wa Bunge kwamba masuala yote nyeti yalenge maslahi ya wananchi na sio maslahi ya mtu mmoja mmoja au kikundi fulani

Mwisho, Suala hili linatoa changamoto kwa mfumo mzima wa demokrasia nchini. Mfumo tulionao wa demokrasia wakilishi haufai tunadai demokrasia shirikishi.

07/02/08

Tenda wema wende zako

Wakati ule kikwete amefanikiwa kuchaguliwa na watanzania kwa zaidi ya asilimia 80 ya kura zote kila mtu alikuwa anajiuliza baraza la mawaziri litakuwaje lakini hakuna aliyekuwa anajiuliza waziri mkuu atakuwa nani .

Kwa hakika waziri mkuu alikuwa ameshajulikana kutokana na historia yenyewe ya raisi na jamaa zake wa karibu , kila mtu alijua ni lowasa bila kubisha .

Lowasa na kikwete wametoka mbali kuanzia chuoni pale UDSM , jeshini , kushika nyadhifa zingine serikalini na katika chama na mambo mengine mengi ya ushirikiano wao ukijumuisha wakina makamba .

Urafiki wao uliendelea kwa muda mrefu mpaka ilipofikia siku ambapo wote kwa pamoja lowasa na kikwete walipoamua kufanya biashara ya kusafirisha ngombe kwenda katika nchi za komoro .

Inasemekana walikuwa na ngombe zaidi ya 7000 hawa ngombe walitakiwa kusafirishwa kwa njia ya maji mpaka visiwa vya komoro , wakafikia makubaliano jinsi ya kusafirisha na mambo mengine .

Kwa kuwa lowasa ndio mtendaji mkuu akaamua kutafuta meli ya bei rahisi kupeleka hawa ngombe , meli yenyewe ilikuwa mbovu baada ya kufanyiwa maangalizi katika bandari ya dare s salaam .

Waziri mkuu pamoja na kujua ile meli ni mbovu akalazimisha ngombe wapakiwe kupelekwa komoro , meli ikaenda komoro kufika njiani meli ikapata matatizo , sehemu yenye ilikuwa ni ngumu kufikiwa kwa njia za karibu za maji .

Wale ngombe wakaanza kufa mmoja mmoja mpaka walipobakia ngombe 1400 , wakati huo lowasa ndio akaanza kutafuta njia za kupeleka chakula katika meli hiyo kwa njia ya ndege lakini alikuwa ameshachelewa sana .

Na hapo ndipo kisa cha kikwete na lowasa kilipoanza , kama unafuatilia vizuri utakumbuka kikwete alikataza wanasiasa kujihusisha katika siasa na biashara au sio ?

Wakati anasema vile alijua fika aliyekuwa anamwambia nae ni waziri mkuu wa wakati huo mh lowassa , lakini alisahau kitu kimoja kwamba na yeye pia ni mfanya biashara tena biashara yake ya mwisho ni hii ya ngombe kusafirishwa kupelekwa komoro hapa napo sijui raisi atueleze nini tumwelewe .

Pamoja na yote haya lowasa anaendesha biashara kadhaa kwa kutumia majina ya watoto wake akina fredy ambaye yuko jijini kwa sasa na richi ambaye yuko nchini afrika kusini kwa sasa .

Sasa basi;-

Kila unapoenda vijana kwa wazee mazungumzo ni Richmond tu , kila sehemu lowasa tu , wengi wanampongeza sana kikwete kwa kazi aliyoifanya ya kumwajibisa lowasa , hawajui kwamba lowassa aliamua kujiuzuru mwenyewe kutokana na hiyo kashfa ya Richmond .

Watanzania bwana na sasa wameshasahau kuhusu EPA , BOT , IPTL , BUZWAGI na kashfa zingine kubwa ambazo ni zaidi ya hii ya Richmond na kwa hakika tume zikiundwa hapa wataondoka wengi .

Jana nilipokuwa natazama TV naona viongozi wa dini nao wanaongelea masuala ya ufisadi bila woga na kujiamini lakini tukumbuke wachungaji hawa hawa ndio wanaomwita lowasa katika matamasha yao ya kuchangia shule na miradi mengine na anachangia pesa nyingi .

Kama lowasa akiwajibishwa na kusema zile hela amepeleka wapi naamini nyingi zitakuwa zimeenda katika kuchangia haya makanisa , hizi shule za makanisa , na taasisi zingine za kikanisa je kanisa liko tayari kurudisha pesa husika ?

Wakati tunataka lowasa arudishe pesa za watanzania , tuwanyooshee vidole kuwaonya viongozi wa dini kwamba nao wanaohusika katika kupokea haya mapesa ya lowasa katika michango yake ya kanisa tunawaomba waelezee hiii michango ya lowasa wameitumia vipi au nao wajiuzuru.

Leo jioni wakati naelekea nyumbani nilipita katika kizuizi Fulani cha gari , wale jamaa wakawa wanataka mchango kwa sababu wametengeneza hiyo bara bara mara dala dala likapita yule konda akawaambia abiria zake
Eehh angalia ile ndio Richmond yao nao wanakula kiulaini .

Na usiku huu hapa nilipo nimeshituka toka usingizini , najiuliza kikwete atatushawishi vipi ili tuweze kuamini baraza lake la mawaziri litakalo tangazwa kesho , kutakuwa hakuna wafanyabiashara wanaokodisha meli mbovu na iharibikie baharini ?

Au atatuletea mawaziri ambao nao wana virichmond vyao huko pembeni ? wanakuja kuendelea na tabia zile zile za kuchota kufukuzwa , kujiuzuru au kuamua kuchoka tu ?

Ngoja tuone kila mtu na kirichmond chake

AJARI MBAYA YAUA SINGIDA


Naaungana na watanzania wenzangu kuwapa pole ndugu zetu walopata ajali iliyotokea Singida, Pia nawaomea wale wote walifaliki dunia.

Mungu azilaze roho za marehemu "Pema Peponi".Ameni

Watu saba wamefariki dunia na wengine 64 wajeruhiwa vibaya na baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori la mizigo.

Ajali hiyo iliyotokea jana kati ya saa 4.30 na saa tano usiku katika Kijiji cha Utaho,tarafa ya Ihanja,wilaya ya Singida vijijini ililihusisha basi la Adventure lenye namba za usajili T.576 ABL aina ya Scania lililokuwa likisafiri kutoka Dar-es-Salaam kwenda Mwanza kugongana uso na lori la mafuta.

Marehemu wawili tu ndiyo mpaka sasa waliokuwa wametambuliwa kwa majina ambao ni Edita Elisha na mwingine ametambulika kwa jina moja tu la mzee Kipara. Hata hivyo habari zaidi zimesema kati ya majeruhi hao waliolazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu, na 31wapo kwenye Hospitali ya Mkoa wa Singida wakati kwenye hospitali ya misheni ya Mtakatifu Maria kuna majeruhi 33. Majeruhi ni pamoja na:-



  1. Amina Twalibu(41) mkazi wa Kigoma,

  2. Robert Wilsoni (37)mkazi wa Kigoma,

  3. Lameck Habibu (48) mkazi wa Kigoma,

  4. Samsoni Shadrack(40) ,mkazi wa Kigoma,

  5. Huseni Simoni (38)mkazi wa kigoma,

  6. Toda Jumanne(26) mkazi wa Kigoma,

  7. Mary Lotenga(18) mkazi wa Kigoma,

  8. Olbert Ernesti(15) mkazi wa Kigoma,

  9. Mwanahawa Twalibu (18)mkazi wa Kigoma

  10. Ramadhani Hassani(41) mkazi wa kigoma.

  11. Bakari (28) mkazi wa Kigoma,

  12. Haruna Juma(54) mkazi wa Kigoma,

  13. Michaeli Julius(23) mkazi wa Kigoma,

  14. Phenusi Jonathani(32) mkazi wa Kigoma,

  15. Hamadi Milongo(43) Kigoma,

  16. Roxima Protasi (26) mkazi wa Ujiji,

  17. Benard Francis (32) mkazi wa Kigoma,

  18. Muhile Emanueli(32) mkazi wa Kigoma,

  19. Nestory Salumu (48) mkazi wa Kigoma

  20. Jeraldi Marcel (34) mkazi wa Kigoma.

Kwa mujibu wa Bi Kaluba wengine ni



  1. Revocatus Philibert (20) mkazi wa Kigoma,

  2. Elia Ntinyaku (31) mkazi wa Kigoma,

  3. Eliasi Eliudi (20) mkazi wa Kasulu,

  4. Renatus Mkarunga (44) mkazi wa Kigoma,

  5. Mikidadi Kongwe(23) mkazi wa Kigoma,

  6. Jumanne Mtaba (30) mkazi wa Kigoma,

  7. Husseni Yasini (34) mkazi wa Kigoma,

  8. Musa Danieli (34) mkazi wa Kasulu,

  9. Mwimbwa Ladiscaus (53) mkazi wa Kigoma,

  10. Bestina Methew (16) mkazi wa Kigoma

  11. Walivyo Athumani (17) mkazi wa Kigoma.