Tuesday, May 20, 2008

BBC Yaongeza muda

BBC Yaongeza muda kwa vijana wafanyabiasharaTarehe ya mwisho ya kuwasilisha michanganuo sasa ni Ijumaa Mei 23.

Vinaja wanaowania kushiriki katika shindano la Faidika na BBC sasa wana muda zaidi hadi Ijumaa Mei 23 kuwasislisha michanganuo yao.

Vijana wenye umri kati ya miaka 16 hadi 24 wana wiki moja zaidi ya kuwaslisha mchanganuo unakaonufaisha jamii yao kwa kutumia zawadi yenye thamani ya dola Elfu Tano za Marekani.

Mchanganuo usizidi maneno 1,500,
lugha ni Kiswahili.

Unaweza kusikia maelezo zaidi ya jinsi ya kuandika mchanganuo bora katika matangazo ya Dira ya Dunia kila siku kutoka Idhaa ya Kiswahili ya BBC na pia kwenye mtandao wetu bbcswahili.com.

Salim Kikeke, Meneja Mradi wa Fadika na BBC 2008, amesema “ Vijana wametuambia wanahitaji muda zaidi kufanyia kazi kile ambacho huenda kikabadili kabisa maisha yao, ndio maana tumeamua kuongeza wiki moja katika tarehe ya mwisho ya kupokea michanganuo”.

Michanganuo inaweza kutumwa kwa njia ya:
E-Mail kwa: faidika@bbc.co.uk,
au kutumwa kwa njia ya posta katika ofisi zetu za kanda.
Faidika na BBC 2008,
Building Maison de la Bible,
Avenue de la Mission,
2eme etage,
En face de PAR,
Bujumbura.

Tanzania
Faidika na BBC 2008,
Jengo la PPF,
Ghorofa ya 8,
Barabara ya Sokoine na Morogoro,
P O Box 79545, Dar es Salaam.

Uganda
Faidika na BBC 2008,
1A, Ruth Towers,Plot 15A,
Clement Hill Road,
P O Box 7620, Kampala.

Michuano ya kitaifa itafanyika kama ifuatavyo: Burundi, Jumatatu Juni 2; Rwanda na DRC, Jumanne Juni 3; Tanzania, Jumatano, Juni 4; Kenya, Ahamisi Juni 5, na Uganda Ijumaa Juni 6.

Washindi sita kutoka katika michuano ya kitaifa, watapambana kuwania zawadi ya kwanza, katika fainali itakayofanyika Uganda, Jumatano Juni 18. Fainali itatangazwa moja kwa moja kupitia Idhaa ya Kiswahili ya BBC na pia kwenye mtandao, katika bbcswahili.com

No comments: