Lipo tatizo la msingi ambalo sisi kama Watanzania au Waafrika tumegoma kabisa kulipa mjadala wa kina. Tunaogopa kabisa kuligusa kwa sababu ambazo kimsingi nilikwishazijadili huko nyuma.
Tatizo ni kwamba nchi hii haina misingi ya kile inachokiamini kwa dhati ambacho watu wake wanaweza kukipigania hata kama watakufa wakiwa wanakipigania. Msingi mkuu sasa hivi ni pesa. Kila mtu anapigania tumbo lake na la watoto wake.
Na kutokana na mlolongo wa matukio, na pia ukweli nilioueleza hapo juu ninaweza kabisa kuvaa joho la Sheikh Yahya Hussein na kutabiri kwa hakika kwamba kabla mwaka huu au kipindi hiki cha kwanza cha Rais Kikwete hakijafika ukingoni basi kutakuwa kumetokea mabadiliko zaidi katika Serikali.
Tuesday, May 20, 2008
Kweli Tanzania Haina Amani? (Hebu kuweni wakweli jamani)
Wageni huko wanakimbilia vituo vya polisi na makanisani kuomba hifadhi kusudi wasiuliwe.Hivi Afrika Kusini imelaaniwa nini? Watu ni wepesi kusahau. Miaka mingapi Tanzania na nchi nyingi za dunia ziliwasaidia waAfrika Kusini mpaka walivyopata Uhuru wao.
BBC Yaongeza muda
BBC Yaongeza muda kwa vijana wafanyabiasharaTarehe ya mwisho ya kuwasilisha michanganuo sasa ni Ijumaa Mei 23.
Vinaja wanaowania kushiriki katika shindano la Faidika na BBC sasa wana muda zaidi hadi Ijumaa Mei 23 kuwasislisha michanganuo yao.
Vijana wenye umri kati ya miaka 16 hadi 24 wana wiki moja zaidi ya kuwaslisha mchanganuo unakaonufaisha jamii yao kwa kutumia zawadi yenye thamani ya dola Elfu Tano za Marekani.
Mchanganuo usizidi maneno 1,500,
lugha ni Kiswahili.
Unaweza kusikia maelezo zaidi ya jinsi ya kuandika mchanganuo bora katika matangazo ya Dira ya Dunia kila siku kutoka Idhaa ya Kiswahili ya BBC na pia kwenye mtandao wetu bbcswahili.com.
Salim Kikeke, Meneja Mradi wa Fadika na BBC 2008, amesema “ Vijana wametuambia wanahitaji muda zaidi kufanyia kazi kile ambacho huenda kikabadili kabisa maisha yao, ndio maana tumeamua kuongeza wiki moja katika tarehe ya mwisho ya kupokea michanganuo”.
Michanganuo inaweza kutumwa kwa njia ya:
E-Mail kwa: faidika@bbc.co.uk,
au kutumwa kwa njia ya posta katika ofisi zetu za kanda.
Faidika na BBC 2008,
Building Maison de la Bible,
Avenue de la Mission,
2eme etage,
En face de PAR,
Bujumbura.
Tanzania
Faidika na BBC 2008,
Jengo la PPF,
Ghorofa ya 8,
Barabara ya Sokoine na Morogoro,
P O Box 79545, Dar es Salaam.
Uganda
Faidika na BBC 2008,
1A, Ruth Towers,Plot 15A,
Clement Hill Road,
P O Box 7620, Kampala.
Michuano ya kitaifa itafanyika kama ifuatavyo: Burundi, Jumatatu Juni 2; Rwanda na DRC, Jumanne Juni 3; Tanzania, Jumatano, Juni 4; Kenya, Ahamisi Juni 5, na Uganda Ijumaa Juni 6.
Washindi sita kutoka katika michuano ya kitaifa, watapambana kuwania zawadi ya kwanza, katika fainali itakayofanyika Uganda, Jumatano Juni 18. Fainali itatangazwa moja kwa moja kupitia Idhaa ya Kiswahili ya BBC na pia kwenye mtandao, katika bbcswahili.com
UFISADI: Viongozi wameiweka CCM kwenye Auto-Pilot?
WENGI wetu tunafahamu kwamba ndege kubwa ya abiria inayosafiri masafa marefu, mathalan London hadi New York, kuna wakati rubani hutegesha mitambo ili ijiendeshe yenyewe (Automatic Pilot).
Kwa kawaida rubani na msaidizi wake hufanya hivyo ili nao wapate nafasi ya kunyoosha miguu, kunywa kahawa au hata kwenda maliwatoni.
Lakini si kila safari unaweza kuiweka ndege katika Auto-Pilot. Ni shurti safari iwe ya masafa marefu.
Aidha, ndege haiwezi kuwekwa Auto-Pilot kabla rubani hajaielekeza mambo fulani fulani; kama vile kule anakotaka ielekee, iende kasi gani na iruke umbali gani kutoka usawa wa bahari.
Kwa habari zaidi bonyeza hapa
Tsvangirai afuta mpango wa kurudi Zimbabwe kutokana na njama ya kutaka kumuuwa.
Baada ya kuwepo nje kwa zaidi ya mwezi mmoja Morgan Tsvangirai alikuwa akitarajiwa kurudi nyumbani leo hii lakini amebadili mipango dakika ya mwisho baada ya kudokezwa juu ya jaribio la kutaka kumuuwa.
Msemaji wa kiongozi huyo George Sibotshiwe amesema wamepokea habari kutoka duru za kuaminika asubuhi hii ya kuwepo kwa mpango wa kumuuwa Tsvangirai. Msemaji huyo anasema kwa hivi sasa hawawezi kusema iwapo mpango huo umeungwa mkono na serikali na habari hizo tayari wamezifikisha kwa wakuu wengine wa nchi na kwamba ni jambo la uhakika kusema kuna ni tishio zito dhidi ya maisha yake na wanaamini kutokana na ushauri wa wanausalama wao isingelikuwa jambo la busara kwa Tsvangirai kwenda Zimbabwe leo hii.
Tsvangirai ambaye mwishoni mwa juma lililopita alisema angelirudi Zimbabwe hivi karibuni alitowa madai kadhaa ya kutaka kuhakikishwa maradio ya uchaguzi huo yanakuwa huru na wa haki ikiwa ni pamoja na kupelekwa nchini humo kwa wanajeshi wa kulinda amani wa kigeni na waangalizi wa uchaguzi.
Whose hands it's in....
This message is now in YOUR hands.
What will YOU do with it?