Tuesday, May 20, 2008

UFISADI: Viongozi wameiweka CCM kwenye Auto-Pilot?



WENGI wetu tunafahamu kwamba ndege kubwa ya abiria inayosafiri masafa marefu, mathalan London hadi New York, kuna wakati rubani hutegesha mitambo ili ijiendeshe yenyewe (Automatic Pilot).

Kwa kawaida rubani na msaidizi wake hufanya hivyo ili nao wapate nafasi ya kunyoosha miguu, kunywa kahawa au hata kwenda maliwatoni.

Lakini si kila safari unaweza kuiweka ndege katika Auto-Pilot. Ni shurti safari iwe ya masafa marefu.

Aidha, ndege haiwezi kuwekwa Auto-Pilot kabla rubani hajaielekeza mambo fulani fulani; kama vile kule anakotaka ielekee, iende kasi gani na iruke umbali gani kutoka usawa wa bahari.

Kwa habari zaidi bonyeza hapa

No comments: