Tuesday, May 20, 2008

Kweli Tanzania Haina Amani? (Hebu kuweni wakweli jamani)



Tanzania tuna Amani jamani.

Unajua ukiongelea ishu ya UFISADI Dunia nzima ni mafisadi na tanzania tunaichukulia mzaha mzaha ndio maana ishu inakwenda inarudi na tanzania tatizo sisi ni masikini ndio maana tuna pigana na Vijisenti alafu na wanoiba wanaiba nyingi kwa wakati mmoja badala ya kuiba kidogo kidogo.


Mna lolote la kuchangia wadau?

Hoja hiyo Mezani................................Kazi kwenu



Wananchi Africa Kusini waua Wageni Nchini Mwao





MMalawi akiokolewa na Polisi!


Leo kuna habari ya fujo zilizotokea huko Afrika Kusini. Wanasema kuwa wananchi wenye hasira wanaua wageni/wahamiaji kutoka nchi zingine amboa wako kwao. Mpaka sasa watu 22 wameuliwa. Kisa eti ni chanzo cha wao kukosa kazi! Wengi ya waliouliwa wanatoka nchi za kiafrika kama Zimbabwe, Mozambique na Malawi.

Wageni huko wanakimbilia vituo vya polisi na makanisani kuomba hifadhi kusudi wasiuliwe.Hivi Afrika Kusini imelaaniwa nini? Watu ni wepesi kusahau. Miaka mingapi Tanzania na nchi nyingi za dunia ziliwasaidia waAfrika Kusini mpaka walivyopata Uhuru wao.


Mnakumbuka Mwalimu Nyerere alivyozuia timu ya Olympiki ya Tanzania kushiriki katika michezo kwa vile Wazungu kutoka Afrika Kusini walikuwa wanashiriki wakati weusi huko wananyanyaswa na Apartheid? Mnakumbuka Dakawa na Mzimbo huko Morogoro? Na tusisahau hao WaSouth Africa walioacha mbegu Bongo!Hebu tukumbuke ni MSouth Africa aliyesababisha ajali iliyotoa roho mpendwa Waziri Mkuu wetu, Edward Moringe Sokoine! Na yule jamaa yuko wapi?

Je, ni moja wa hao wanaotaka kuona waBongo huko wanauliwa!Askofu Desmond Tutu amewaomba waache kuua watoto wa watu waliowasaidia kutoka kwenye mikono ya Apartheid. Ni aibu!



No comments: