Saturday, March 1, 2008

safari hii ni mavazi ya ngozi


safari hii ni mavazi ya ngozi
Siku ya Wanawake Duniani Machi 8, mwaka huu inatarajiwa kupambwa na mavazi ya ngozi za mbuzi, magome ya miti na magunia kutoka kwa mwanamitindo Fatuma Amour. Akiongea na Darhotwire , mbunifu huyo alisema sherehe hizo zitafanyika katika ukumbi wa Movenpick jijini na kaulimbiu yake ni ‘heshima kwa akina mama’.


Aidha, alisema hafla hiyo pia itatumika kuwaburudisha watu watakaofika kwa lengo la kutuliza nyoyo zao, huku wakibadilishana mawazo na kufahamishana mambo mbalimbali. Alisema, ili kutoa burudani ya heshima na kuhakikisha siku hiyo inakuwa ya kupendeza, kutakuwapo na bidhaa kama mikoba na malapa vilivyobuniwa katika mtindo wa kiutamaduni. Alisema, vikundi vya burudani vitakavyotumbuiza siku hiyo ni Unique Sisters na kikundi cha sanaa cha Saidi Comorien. Mwaka jana tulisherehekea siku hii kuambiwa tubebe vikapu na tuachane na mifuko ya karatasi ili tuweze tunza mazingira...mwaka huu ni mwenzo wa ngozi Hallow!!


No comments: