Tuesday, February 12, 2008

Tanzania ya Nyerere: Mafunzo ya maendeleo, umoja na amani

Mgomo wa 6 wa Wanawake Duniani – Machi 8 2005
Wapendwa ndugu zangu,
Komesha Umasikini na Vita – Wekesha katika Kutunza na siyo Mauaji!
Malipo kwa kazi zetu na sawazisha malipo kwenye soko la Dunia
Kila iliposherehekewa Siku ya Kimataifa tangu Mwaka 2000,Wanawake katika zaidi ya Mataifa 60 wametumia kila hatua za pamoja kuanzia ngazi ya chini wakiitaka jamii iwekeze katika kutunza badala ya mauwaji, na kwamba fedha zinazoharibiwa kugharimia vita zingetumiwa badala yake kutimiliza mahitaji ya jamii. Mgomo huu umezidi kua imara katika kipindi cha miaka mitano,hususan katika Mataifa ya kusini mwa Dunia, ambapo wanawake na pia idadi ya wanaume inayozidi kuongezeka, kwa pamoja wanazingatia hatua hizi kila kukicha. Tumejionea jinsi manufaa ya ushirikiano wa kimatifa bila kujali mipaka .

Kupinga vita na kukomesha umasikini ni masuala mawili yasiyotengeka. Janga la hivi karibuni la Tsunami liliua karibu ya watu 300,000, lakini kila siku watu wanauawa kwa njaa,magonjwa, joto linalosababishwa na uharibifu wa mazingira pamoja na vita-yote yanayosababishwa na utawala wa uroho wa pesa na soko. Serikali pamoja na wapenzi wao wadhamini wa Kimataifa wanazungumzia bila kutimiza jinsi ya kukomesha umasikini lakini hawajawahi kutaja uwezekano wa kutukabidhi fedha tunazohitaji. Ni sisi wenyewe, tukianza na wanawake walezi wanaohangaika kila kukicha kuhifadhi maisha, juhudi zisizo lipiwa, ndiyo tutaweza kutekeleza mabadiliko haya. Mgomo ndiyo mfumo wetu wa kujiandalia lengo hili.
Madai ya Mgomo
· Malipo kwa kazi zote za huduma –katika mishahara,pensheni ya uzeeni,ardhi na njia nyingine za mapato.Nini la thamani kuliko malezi ya watoto na kuwatunza wengine? Wekeza katika uhai na mahitaji ya kimaisha,siyo bajeti ya majeshi au magereza.
· Usawa wa malipo kwa wote,wanawake kwa waume katika soko la Kimataifa.
· Upatikanaji wa chakula kwa mama anayenyonyesha, malipo ya likizo ya uzazi na likizo ya kujifungua. Komesheni kutuadhibu kwa sababu ya kuwa wanawake.
· Msilipe madeni ya Dunia ya Tatu’ Hatudaiwi ila tunawadai wao.
· Upatikanaji wa maji safi,huduma za afya,malazi, usafiri na elimu.
· Nguvu na Teknolojia zisizo haribu mazingira ambazo hufupisha saa za kazi.Wote tunahitaji majiko ya kisasa,majokofu, mashine za kufulia,kompyuta na mda wa kupumzika!
· Ulinzi a hifadhi dhidi ya fujo na unyanyasaji, pamoja na unaofanywa na watu katika familia na viongozi walio madarakani.
· Uhuru wa kusafiri. Hela inaruhusiwa kusafirishwa bila pingamizi,kwanini watu wasiwe na uhuru kama huo?

No comments: