Swali
Kwa kuwa muda mrefu sasa, wananchi waishio Londrosi West Kilimanjaro katika Wilaya ya Siha, wamekuwa wakitaabika kutokana na ubovu wa barabara itokayo Ngare Nairobi Londrosi Gate; na kwa kuwa ubovu huo unakwamisha shughuli za kiuchumi hasa kwa upande wa watalii wanaotaka kupanda Mlima Kilimanjaro:-
(a) Je, ni Mamlaka gani inayotakiwa kushughulikia barabara hiyo?
(b) Je, ni hatua gani zinachukuliwa na Serikali kurekebisha hali hiyo?
ANSWERS TO PRINCIPAL QUESTION
Answer From Hon. Dr. Milton Makongoro Mahanga INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT
NAIBU WAZIRI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aggrey D. J. Mwanri, Mbunge wa Siha, lenye sehemu (a) na (b), kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, barabara ya Ngare Nairobi - Londrosi Gate inashughulikiwa na Mamlaka mbili tofauti; sehemu ya Ngare Nairobi hadi Simba Farm yenye urefu wa kilomita 1.5 kwa upande moja ambayo ni barabara ya Mkoa (Sanyajuu – Kimwanga) iko chini ya uangalizi wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Kilimanjaro na kwa upande mwingine, barabara itokayo Simba Farm – Londrosi Gate yenye urefu wa kilomita 10, iko chini ya uangalizi wa KINAPA na kampuni ya West Kilimanjaro.
Monday, May 26, 2008
Maswali na Majibu Bungeni 26/5/2008
Bonyeza hapa - Muendelezo wa majibu
at
3:34 PM
Posted by
Mwanaharakati
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment