Monday, May 26, 2008

Maswali Bungeni 26/5/2008

1. Kwa kuwa ni muda mrefu sasa ujenzi wa nyumba za makazi ya Polisi Kambi ya Finya, umesimama na kwa kuwa nyumba za makazi ya polisi zilizopo police line Wete ni mbovu sana, zimechakaa na zinavuja mno wakati wa mvua hali ambayo inasababisha usumbufu mkubwa na kuhatarisha usalama kwa familia zinazoishi humo na kwa kuwa polisi wengi na hasa wa vyeo vya chini wana ari ya kujenga nyumba binafsi za kuishi lakini kipato chao ni kidogo:-

(a) Je, Serikali itamalizia lini ujenzi wa nyumba za polisi Kambi ya Finya?

(b) Je, ni lini Serikali itazifanyia matengenezo nyumba za Police Line ili ziwe na hali nzuri?

(c) Je, Serikali haiwezi kuwasiliana na taasisi za fedha nchini ili polisi wapatiwe mikopo ya kujenga nyumba zao za binafsi?

bonyeza hapa kwa- majibu

2. Kwa kuwa, Wananchi wa Mji wa Mererani wanajishughulisha na biashara na uchimbaji wa madini ya Tanzanite, lakini wamekuwa wakipata taabu ya barabara kati ya Mererani na KIA; na kwa kuwa Rais wa Awamu ya Tatu na Awamu ya Nne walipoiona hali hiyo ngumu waliahidi kujenga barabara hiyo isiyozidi kilomita 20 kwa kiwango cha lami:- Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kujenga barabara hiyo muhimu sana kiuchumi, kutimzia ahadi zilizotolewa na Ma-Rais hao.

Jibu kutoka kwa Mh. Celina Ompeshi Kombani REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT

NAIBU WAZIRI alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, napenda kujibu Swali la Mheshimiwa Chrisopher Ole-Sendeka Mbunge wa Simanjiro kama ifuatavyo. Majibu


3. Kwa kuwa Serikali ina mikakati mizuri ya kuwawezesha wananchi hususan wanawake kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuwapatia mikopo ya kufanyia biashara ndogo ndogo; na kwa kuwa Mkoa mpya wa Manyara una matatizo mengi makubwa ya mazingira ya kufanyia biashara hizo ikiwa ni pamoja na elimu ya ufahamu, kero za maji, uhaba wa Zahanati kwa baadhi ya vijiji na kutokuwepo na hospitali ya Mkoa.

(a) Je, Serikali ina mipango gani ya upendeleo kwa Mkoa wa Manyara ya kuboresha Mazingira chini ya Mpango wa MKUMBITA?

(b) Je, Serikali itafikisha lini mradi wa SELF Mkoani Manyara ikizingatiwa kuwa hakuna taasisi za fedha zinazofikisha huduma huko zaidi ya SACCOS zilizoanza hivi karibuni?

Jibu kutoka kwa Mh. Dr. Batilda Salha Burian PLANNING, ECONOMY AND EMPOWERMENT

NAIBU WAZIRI alijibu: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Martha Umbulla, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- Majibu

No comments: